Rais Kenyatta
kwa upande wake bila kutaja CCM, alisema anaamini Watanzania wataendelea
kuiunga mkono Serikali na chama ambacho kimeweza kuwaletea, amani,
umoja na maendeleo.
Marais hao
walitoa kauli hizo katika mji wa Taveta wakati wa sherehe za uzinduzi wa
ujenzi wa barabara ya Taveta –Voi – Mwatete nchini Kenya, yenye urefu
wa kilomita 98.4 kwa kiwango cha lami.
Ujenzi wa
barabara hiyo unaofadhiliwa na Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB), kwa
Sh8.4 bilioni za Kenya (takriban Sh168 bilioni), ulianza Mei 2014 na
utakamilika Mei 2017.
Rais Kikwete
alimweleza Rais Kenyatta pamoja na wananchi wa nchi hizo mbili
waliohudhuria sherehe hizo kwamba amefurahi kupata fursa ya kuwaaga
Wakenya.
“Rais
amenialika wakati mzuri. Baada ya siku 21 kutoka leo (jana) tutakuwa
tunapiga kura kuchagua Rais mpya,” alisema na kubainisha kuwa wananchi
hao walikuwa na shauku la kujua rais ajaye ni nani.
“Mnaniuliza
yupi? Atatoka chama changu tu, hilo sina wasiwasi nalo na Watanzania
wanajua hilo. Hii ni nafasi nzuri ya kuja kuwaaga wenzangu wa Kenya,”
alisema Rais Kikwete, kauli iliyoibua makofi na vicheko.
Rais Kenyatta
alimtakia kila la heri Rais Kikwete wakati anapojiandaa kuondoka
madarakani akimtaka amsaidie kuonyesha njia ni kazi gani marais wastaafu
wanatakiwa kufanya wanapostaafu urais.
“Sisi pia
utatuonyesha barabara ni kazi gani rais mstaafu huwa anafanya wakati
wetu ukifika ili tujue tunaelekea wapi. Tunakutakia kila la heri katika
kampeni za uchaguzi,” alisema.
Katika
Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, CCM kimemsimamisha Dk John Magufuli
kupeperusha akichuana zaidi na mgombea wa Chadema na Ukawa, Edward
Lowassa na pamoja na wengine sita.
Akizungumzia
miradi ya barabara inayoendelea Kenya na Tanzania, Rais Kikwete alisema
barabara hizo zimefanya biashara kati ya Kenya na Tanzania kwa miaka
mitano kuongezeka kwa asilimia 40. “Barabara hii ikikamilika itaongeza
asimilia nyingine 10. Nimekuja tu kuwaaga, lakini nimekuja
kuwahakikishia kuwa Tanzania itaendelea kuwa rafiki wa Kenya,” alisema.
Alisema ujenzi
wa barabara hiyo ni muhimu hasa kwa wananchi wa mikoa ya kaskazini na
kukamilika kwake kutafupisha muda wa safari hadi kufikia saa 2.30 kutoka
saa 14.
Mkurugenzi wa
AfDB Afrika Mashariki, Gabriel Negatu, alisema imetoa mkopo wa Dola 1.5
milioni kwa ajili ya miradi hiyo mikubwa ya barabara Kenya na Tanzania.
-mwananchi
-mwananchi
0 comments