Photo source: unkown

Watu milioni moja walitakiwa kuacha makazi yao na takriban watu 11 walipoteza maisha baada ya tetemeko lenye ukubwa wa kipimo cha ritcha 8.3 kupiga Jumatano usiku. 
Tukio hilo limechangia serikali kutangaza hali ya dharura
Mji wa pwani, Coquimbo, mawimbi ya futi 15 yalipiga pwani. Mawimbi madogo ya Tsunami yalipiga mpaka Alaska.
Tetemeko hili ambalo ndilo kubwa zaidi duniani mwaka huu lilidumu dakika tatu.
 Rais Michelle Bachelet alitembea Coquimbo Alhamisi.
Kijiji cha Tongoy kiliharibiwa, na zaidi ya nyumba 500 ziliharibiwa vibaya, vikosi vya kupambana na dharura vimeeleza.
 Takriban nyumba 90,000 hazina umeme.