By Dk Shita Samweli; 0763-296752
Ukijaribu kuwahoji wanaume walio wengi endapo wanatamani kuongeza maumbile yao ya uzazi, kwa maana ya urefu na upana, majibu mengi ni “ndiyo.”
Ni jambo ambalo limeenea katika jamii nyingi na kuwaathiri wanaume kisaikolojia. Wengi wanaamini maumbile makubwa ndiyo yanakupa uwezo wa kumfikisha kileleni mwenza.
Vilevile huamini kuwa maumbile hayo ndio yanayoleta msisimko kupita kiasi na kuamini wataonekana rijali na watawavutia wanawake wengi.
Pasipo kufahamu kuwa msisimko wa kilele cha tendo ni ujuzi wako binafsi, kutumia akili na kutumia viungo vyako vya mwilini kuweza kuleta msisimko. Hawajui pia, afadhali kuwa na uume wa wastani kuliko mkubwa uliopitiliza kwani unaweza kumsababishia maumivu mwenza wake na asifurahie tendo hilo na anaweza pia kupata hofu kwa ukubwa huo.
Jambo usilolijua ni sawa na usiku wa giza. Laiti kama kungekuwa na njia salama za kunenepesha na kurefusha maumbile katika huduma za afya, gharama za kuchangia matibabu zingekua maradufu.
Kwa sababu wanaume wengi wanaodhani wana maumbile madogo ya uume wangemiminika kwenda kutibiwa tatizo hilo. Wizara ya Aafya na Ustawi wa Jamii na Mamlaka ya Chakula na Dawa ya Tanzania (TFDA) na hata zile za nchi zilizoendelea ikiwamo Uingereza na Marekani na Shirika la Afya Duniani (WHO), vyuo vikuu vinavyofanya mamia ya utafiti, hakuna mahala wamepitisha na kupendekeza dawa au kifaa tiba kwa ajili ya kurefusha na kunenepesha uume kwa watu wazima.
Njia chache tu ambazo wanakubali kuwa zinaweza kusaidia angalau kidogo kuongeza lakini isiyozidi nchi moja, njia hizo ni pamoja na kupunguza unene.
Watu wanene kupitiliza, chini ya kitovu shina la uume humezwa na mafuta na nyama zingine zilizorundikana na hivyo kupunguza urefu wa uume kutokea katika shina.
Hivyo kupunguza unene kwa njia ya vyakula na mazoezi inakubalika. Vilevile kwa njia za upasuaji ikiwamo wa kupunguza mafuta ya eneo hilo.
Vitu vinavyojulikana kutumika kiholela kunenepesha na kurefusha uume ni pamoja na vidonge, sindano, virutubisho, mashine maalumu, upasuaji wa kupandikiza, vifaa vyakufanyisha mazoezi uume, mafuata, cream za kupaka uumeni na mitishamba.
Vitu hivi vinauzwa kisiri katika baadhi ya maduka ya dawa baridi, kwa njia ya mtandao. Wapo wanaopita mtaani wakizuiza mikononi na wapo wanauza kwa kujitangaza katika magazeti.
Hata hivyo, kati hivyo nilivyotaja, hakuna vinavyofanya kazi kwa ufanisi na kukidhi vigezo vya kitaalamu kupitia vyombo vikubwa vya matibabu na uthibiti wa magonjwa, likiwamo Shirika la WHO.
Kwa sababu hakuna tafiti za kisayansi kuthibitisha ubora, ufanisi na usalama wa vitu hivyo. Ni kweli vingine vinaweza kukusaidia lakini ndio vinakuacha na madhara makubwa hapo baadaye.
Madhara hayo ikiwamo kukosa au kupungua nguvu za kiume, kupata michubuko, kuvunjika misuli ya uume, madhara ya neva na kupata maumivu sugu wakati wa kujamiiana. Tafiti inaonyesha wanaume wengi wanajikuta wakinasa na kununua vifaa hivi kirahisi kwa sababu ya kuathirika kwao kisaikolojia, hujikuta na shauku iliyopitiliza ya kuongeza maumbile. Ukijaribu kuwadadisi unakuta wengi wao hawajawahi hata kufika huduma za afya kuomba ushauri wa tatizo hilo. Wengi wanaojihisi wana uume mdogo hugundulika kuwa hawapo chini ya nchi tatu, baada ya uume kusimama.
Moja ya tafiti iliwahi kugundua kuwa wanaume wanaotaka upasuaji wa uume ili kurefushwa, huwa wana tatizo la kiakili lijulikanalo kitaalam penile dysmorphic disorder.

CHANZO;MWANANCHI