![]() |
Katibu Mkuu wa Chadema,Dk.Wilbroad Slaa |
Wakati vyama vya upinzani vikijiandaa kuzindua kampeni zake katika
uwanja wa Jangwani hapo kesho ili kumnadi mgombea wake wa urais, Mh. Edward
Lowassa, duru zinaeleza kuwa huenda Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Wilbroad
Slaa akahudhuria uzinduzi huo.
Mmoja kati ya viongozi wa Chadema ambaye
alinukuliwa na
gazeti moja kubwa nchini huku akitaka jina lake lifichwe, alinukuliwa akisema “Zipo taarifa za chinichini kuwa Dk. Slaa
atahudhuria uzinduzi, hatujui zina ukweli kiasi gani na atashiriki kama
Katibu Mkuu au mgeni mwalikwa, kama atahudhuria, atatusaidia sana na
asipokuja suala lake litaendlea kuwachanganya wafuasi wa Chadema,”
alinukuliwa kiongozi huyo wa Chadema.
Haijafahamika kama taarifa hizo ni
za kweli au uzushi ila kwa kuwa hata uamuzi wa kumkaribisha Edward Lowassa
kujiunga na Chadema ulifanywa kuwa siri kubwa kwa viongozi wachache sana
takribani miezi mitatu kabla.
Dk. Slaa alijiweka kando na
harakati za kampeni za Chadema na Ukawa kwa ujumla baada ya kutoridhia
uamuzi wa chama chake kumkaribishaLowassa ambaye awali walikuwa
wakimtuhumu kuwa katika orodha ya mafisadi nchini.
Ukawa
wanatarajia kufanya uzinduzi wao kesho (Agosti 29) katika viwanja vya
Jangwani ikiwa ni wiki moja baada ya CCM kuutumia uwanja huo kwa
shughuli hiyohiyo.
chanzo:PressTz
0 comments